China imewahamisha maelfu ya watu na kuamuru takriban miji 10 kufunga shule na baadhi ya biashara huku kimbunga kikali zaidi kwa mwaka kikitarajiwa katika pwani yake ya kusini.
Kimbunga hicho kinatarajiwa kupiga katika mkoa wa Guangdong nchini China siku ya Jumatano, ambapo takriban watu 370,000 wamehamishwa hadi sasa, huku mamlaka ikionya hali itakuwa mbaya.
Kimbunga Ragasa kimepewa jina la “Mfalme wa Vimbunga” na shirika la hali ya hewa la China na kinatarajiwa kuelekea kaskazini mwa Vietnam katika siku zijazo, na kinaweza kuathiri mamilioni ya watu.
Siku ya Jumanne, rafu za maduka makubwa huko Hong Kong zilikuwa tupu watu wakinunua mkate, mboga mboga, nyama na tambi za papo hapo huku wakazi wakijiandaa.
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hong Kong ulisema unatarajia “idadi kubwa ya safariza ndege” kuanzia siku ya Jumanne hadi siku inayofuata.
Katika miji ya kusini mwa China, wamiliki wa maduka walirundika mifuko ya mchanga mbele ya maduka yao ili kujiandaa na kuwasili kwa kimbunga, huku wakaazi katika maeneo ya mabondeni karibu na mbele ya bahari wakiwa na wasiwasi haswa juu ya mawimbi ya maji.
Wengi pia wamefunga madirisha ya nyumba na biashara zao, wakitumaini kuzuia uharibifu kutokana na upepo.
Bado haijabainika ni kwa kiasi gani mabadiliko ya tabia nchi yamechangia kimbunga cha Ragasa. Lakini joto linaloongezeka duniani linatarajiwa kuongeza dhoruba na vimbunga kuwa vikali zaidi, kulingana na wanasayansi wa Umoja wa Mataifa.
Hiyo uwepo wa upepo mkali, mvua kubwa na hatari ya mafuriko katika maeneo ya pwani.
Kimbunga Ragasa kilipita katika kisiwa cha Taiwan usiku wa jana, takriban watu sita walijeruhiwa na zaidi ya safari 100 za ndege za kimataifa kufutwa.
Ragasa kilipita katika kisiwa cha mbali kaskazini mwa Ufilipino siku ya Jumatatu, na kuua mtu mmoja huku maelfu ya familia zikihamishwa kabla ya kimbunga hicho kuanguka.
Shule na ofisi za serikali zilifungwa, ikiwa ni pamoja na katika mji mkuu wa Manila.
Kimbunga Ragasa kinavuma kwa upepo mkali wa hadi kilomita 285 kwa saa (177mph) katika kiwango chake cha juu siku ya Jumatatu, na kimesababisha mafuriko, mawimbi ya dhoruba na maporomoko ya ardhi katika nchi hiyo.
Kimbunga kikuu cha Mangkhut cha 2018 – ambacho ndio kikubwa kikali zaidi kupiga eneo Hink Kong – kilijeruhi watu 200, kuzamisha meli na miundombinu kuharibika, na kuacha hasira ya HK $ 4.6bn ($592m: £438m).
Mnamo mwaka wa 2017, kimbunga Hato kilisababisha mafuriko makubwa na kujeruhi zaidi ya watu 100 katika jiji hilo.
